ELCT Press Release

Date: July 14, 2015
Press release No. 003/07/2015

close window


Mkutano Mkuu ni Makumira tena

Mkutano Mkuu wa 19 wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) utafanyika Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira (TUMA) kilichopo Arusha 12 - 14 Agosti 2015.

Katibu Mkuu wa KKKT, Bw. Brighton Killewa, amesema hivi karibuni kwamba Mkutano huo Mkuu utaongozwa na Neno Kuu: “Jitahidi kuuhifadhi umoja wa roho katika kifungo cha amani” (Efeso 4: 3).

Mkutano Mkuu hufanyika kila baada ya miaka minne na lengo ni kupokea, kujadili taarifa mbalimbali na kuweka malengo na mwelekeo wa miaka ijayo.

Mkutano Mkuu pia huchagua viongozi mbalimbali kama Mkuu wa KKKT, Mwandishi na Wajumbe wa Halmashauri na Kamati mbalimbali za Kanisa.

Somo la Biblia litaongozwa na Askofu Mstaafu Dkt. Hance Mwakabana Na Somo hilo litaanza kutolewa siku ya ufunguzi na kuendelea kwa siku zote za Mkutano.

Pia wajumbe watashiriki warsha ambapo mada mbalimbali zitawasilishwa na kujadiliwa. Mada zitaongozwa na kauli mbiu isemayo: “umoja na utambulisho wetu”.

==================================================
Elizabeth Lobulu
Communication Coordinator,
Evangelical Lutheran Church in Tanzania
Box 3033, ARUSHA, Tanzania.
Phone: +255-27-250-8856/7
FAX: +255-27-254-8858
E-mail: Elizabeth Lobulu <ELobulu@elct.or.tz>

Close this window

For more information contact:

Elizabeth Lobulu
Communication Desk Officer, ELCT
E-mail: ELobulu@elct.or.tz