Music Recording |
|
![]() Musicians at the production
Drop us an e-mail ! |
some memos if you come to be recorded: Kumbuka mambo yafuatayo wakati wa kufanya booking au wakati wa kurekodi kwayaSauti ya Injili * Fika katika saa 2 na nusu mpaka saa 3 kamili asubuhi.siku ya kurekodi * Fika na vyombo ulivyozoea kutumia na kwaya yako kmf keyboard,gitaa nk * Hakikisha vyombo vyako vinafanyakazi (nyuzi za gita, adapta, betri nk ) * Kumbuka bites na vinyvaji * Kama unapenda kutumia vifaa vya SYI (Kinanda, Gitars) wasiliana na idara utakayoelekezwa na mhudumu. * Kwaya itaanza kurekodiwa saa nne kamili asubuhi,kuanzia saa tatu hadi saa nne kwaya itaruhusiwa kufanya mazoezi. * Kuna njia mbili za kurekodi. Kama kuna kwaya nzima tunarecord yote moja kwa moja pamoja na vyombo. Kwa mwimbaji mmoja atarekodiwa kwa tracks. * Kwaya ikishaingia studio hairuhusiwa kutoka mpaka kumaliza kurekodi. Hii inasaidia tusifaye setup upya kila wakati pia sauti za waimbaji kutokubadilika. Lakini kuna breki mbali mbali sehemu ya studio. * Tunategemea kumaliza kurekodi saa 8. Kama unapenda kurekodi album 2 tafadhali fanya booking kwa siku 2. * Sisi kama staff ya SYI tunategemea kuwa kwamba utafanya maandalizi mazuri. * Kama utapenda ushauri ya kimuziki tafadhali piga simu namba 0754 28 68 30 au 0784 25 42 43. Kuna uwezekano wa kupata ushauri wakati wa mazoezi huko ulipo! * Kama una Soundtrack kama MIDI File , .WAV file, au digital file tofauti kwenye DAT nk, tafadhali onana na fundi kwa maelekezo kabla hujaja kurekodi. KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA Evangelical Lutheran Church in Tanzania |